Most Popular

Mwanamke aliyekataa kuvua Hijabu afukuzwa kazi Ujerumaini

Mwanamke mmoja aliyekuwa masomoni kwenye mji wa Luckenwalde nchini Ujerumani amefukuzwa kazi kwa kukataa kuvua Hijabu.

Gazeti la Daily Mail limeripoti habari hiyo na kusema kuwa, mwanamke huyo Muislamu mwenye asili ya Palestina, alifukuzwa kazi jana Alkhamisi katika siku yake ya kwanza kuripoti kazini katika manispaa ya Luckenwalde, mkoani Brandenburg, Ujerumani.

Meya wa mji wa Luckenwalde, Elisabeth Herzog-von der Heide ameliambia gazeti la Daily Mail kuwa wameamua kumfuta kazi mwanamke huyo Muislamu baada ya kukataa kuvua Hijabu.
Meya wa mji wa Luckenwalde, Elisabeth Herzog-von der Heide

Amedai kuwa, kuvaa vazi la Hijabu katika ofisi za meya wa mji huo, eti kutaiopotezea itibari ya kijamii ofisi yake.

Amedai pia kuwa, masuala ya kiitikadi hayapaswi kusababisha machafuko na wasiwasi katika jamii.

Hata hivyo hatua ya meya huyo imelalamikiwa na baadhi ya idara za serikali pamoja na taasisi za kijamii za Ujerumaini na kusema kuwa hatua hiyo ni kinyume cha sheria na kuitaka manispaa ya mji huo ulioko umbali wa kilomita 70 kusini mwa Benlin, iache ubaguzi wa kidini katika kuajiri wafanyakazi wake.
Posted By: MJOMBA ZECODER

Mwanamke aliyekataa kuvua Hijabu afukuzwa kazi Ujerumaini

No comments:

Post a Comment

About Us

Advertisment

Like Us

© HABARI KUHUSU WAISLAMU All rights reserved | Theme Designed by Mjomba Computers Published.. Blogger