26.08.2016
Waislamu Marekani waendeleza kampeni za kuutangaza vizuri Uislamu
![]() |
Add caption |
Wanachuo Waislamu wa Chuo Kikuu cha jimbo la Wisconsin nchini Marekani
wameanzisha kampeni ya kugawa chakula kwa watu wasio na makazi wa mji wa
Madison ili kuwapa fursa ya kuujua Uislamu na kuuliza maswali kuhusiana
na dini hiyo ya Mwenyezi MunguENDELEA
26.08.2016
Ndugu watatu Waislamu wateremshwa kwenye ndege kwa kutuhumiwa kuwa wanachama wa Daesh
Ndugu watatu Waislamu raia wa Uingereza wamefikwa na mkasa wa
kuteremshwa kwenye ndege katika uwanja wa ndege wa London na kuhojiwa
kwa muda wa saa nzima baada ya abiria wenzao kuwatuhumu kuwa ni
wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh.ENDELEA
26.08.2016
Mwanamke aliyekataa kuvua Hijabu afukuzwa kazi Ujerumaini
Mwanamke mmoja aliyekuwa masomoni kwenye mji wa Luckenwalde nchini Ujerumani amefukuzwa kazi kwa kukataa kuvua Hijabu.
![]() |
Meya wa mji wa Luckenwalde, Elisabeth Herzog-von der Heide |
Gazeti la Daily Mail limeripoti
habari hiyo na kusema kuwa, mwanamke huyo Muislamu mwenye asili ya
Palestina, alifukuzwa kazi jana Alkhamisi katika siku yake ya kwanza
kuripoti kazini katika manispaa ya Luckenwalde, mkoani Brandenburg,
Ujerumani.ENDELEA
22.08.2016
IRANI:
Ayatullah Khamenei:Msikiti ni kituo cha kuandaa mazingira kwa ajili ya kuleta ustaarabu wa Kiislamu.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, msikiti
unapaswa kuwa kituo cha kumjenga mwanadamu kukabiliana na adui, kuujenga
moyo kimaanawi na kidunia, kuongeza muono na kuandaa mazingira kwa
ajili ya kuleta ustaarabu wa Kiislamu.
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu akiendelea kuzungumzia
umuhimu wa msikiti amesema kuwa, katika historia ya Uislamu, msikiti
ulikuwa ni makao makuu ya mashauriano, ushirikiano na sehemu ya kuchukua
maamuzi kuhusiana na masuala muhimu ya kijamiii, kisiasa na kijeshi.ENDELEA
21.08.2016
Wanawake Waislamu kutoka Iran, Misri washinda medali katika Taekwondo Olimpiki Rio
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Misri zimepata medali zao za kwanza za
mashindano ya taekwondo ya wanawake katika michezo ya Olimpiki ya Rio,
2016.
Kwa mujibu wa mwandishi wetu, wanawake wachanga kutoka nchi za
Kiislamu ni nguvu ibuka katika taekwondo na hilo limebainika kufuatia mafanikia
makubwa waliyopata katika michezo ya Olimpiki ya Rio di Janeiro nchini Brazil
mwaka huu wa 2016.ENDELEA
19.08.2016
Waislamu waandamana Marekani kulaani udhalilishwaji wa wanawake wawili wa Kiislamu.
Waislamu wa eneo la Rogers Park mjini Chicago nchini Marekani wamefanya
maandamano kulaani vitendo vya udhalilishaji walivyofanyiwa wanawake
wawili wa Kiislamu mjini hapo.
Habari kutoka mjini Chicago zimearifu kwamba wakazi wa eneo hilo
wakiwemo Waislamu na wasio Waislamu, sambamba na kumiminika mabarabarani
kulaani kitendo hicho, wameitaka polisi ikitaje kitendo hicho kuwa ni
kosa la kuchukiza sanjari na kuanzisha uchunguzi juu yake. Aidha
waandamanaji hao mbali na kupiga nara dhidi ya vitendo vya udhalilishaji
wanavyofanyiwa Waislamu, wameonyesha machungu yao kwa ajili ya wanawake
hao wa Kiislamu.ENDELEA
19.08.2016
Utafiti: Uislamu ndiyo dini inayokuwa kwa kasi zaidi duniani
Utafiti uliofanywa na kituo cha utafiti cha Pew Research Center cha
Marekani umeonyesha kuwa, Uislamu utasalia kuwa dini yenye kukuwa kwa
kasi zaidi duniani katika kipindi cha miongo kadhaa ijayo.
Shirika la Bloomberg limeripoti kuwa, utafiti wa kituo cha Pew chenye
makao makuu yake mjini Washington umebainisha kuwa, idadi kubwa ya watu
wanavutiwa na Uislamu kutokana na mafundisho yake, haswa kuhusu miamala
na bishara za halali. Utafiti huo umesema kuwa, idadi kubwa ya watu
wanavutiwa na namna Uislamu unavyofundisha juu ya kupata kipato cha
halali na kujihusisha na biashara na uwekezaji unaofuata sheria na
mafundisho ya Qurani tukufu.ENDELEA
19.08.2016
Waziri Mkuu wa Ufaransa aunga mkono marufuku ya 'burqini
![]() |
Burqini |
Waziri Mkuu wa Ufaransa ameunga mkono hatua ya mameya wa miji minne
nchini humo kupiga marufuku vazi la stara la kuogelea linalovaliwa na
wanawake wa Kiislamu linalofahamika kama 'burqini'.
Manuel Valls amesema vazi hilo haliendani na thamani, utamaduni na desturi ya Wafaransa na hivyo ni sawa kwa wanawake wa Kiislamu kutoruhusiwa kulivaa wanapoenda kuogelea kwenye fukwe za umma.ENDELEA
Manuel Valls amesema vazi hilo haliendani na thamani, utamaduni na desturi ya Wafaransa na hivyo ni sawa kwa wanawake wa Kiislamu kutoruhusiwa kulivaa wanapoenda kuogelea kwenye fukwe za umma.ENDELEA
19.08.2016
Wafuasi 418 wa Ikhwanul Muslimin wahukumiwa adhabu kali na mahakama ya kijeshi ya Misri.
Mahakama ya kijeshi ya Misri imetoa hukumu ya vifungo vya kuanzia miaka miwili hadi maisha jela kwa watu 418 ambao ni wanachama na wafuasi wa harakati ya Kiislamu ya Ikhwanul Muslimin.Mahakama hiyo imetoa hukumu kwa watu 350 bila ya wenyewe kuwepo mahakamani za kuanzia miaka 25 hadi kifungo cha maisha jela. Washtakiwa 68 waliokuwepo mahakamani wamehukumiwa vifungo vya kati ya miaka miwili hadi kumi jela.ENDELEA
18.08.2016
Wanariadha waonyesha nguvu za Uislamu katika Olimpiki Rio
Wanariadha watatu Waislamu wameonyesha nguvu na taswira nzuri ya Uislamu katika michezo ya Olimpiki ya Rio, 2016.
Kwa mujibu wa
mwandishi wa chanzo chetu cha habari, jarida la Time limechapisha taswira za baadhi ya wanariadha
Waislamu ambao wamepata medali katika michezo ya Olimpiki inayoendelea mjini
Rio nchini Brazil. Pamoja na kuwepo chuki dhidi ya Uislamu, wanariadha Waislamu
wamewasilisha taswira nzuri katika michezo ya RioENDELEA
18.08.2016
Mashindano ya Qur’ani ya msimu wa joto yameanza mjini Bidiya nchini Oman.ENDELEA
18.08.2016
Mwanamke wa kwanza Mwislamu kuchaguliwa kugombea ubunge Minnesota, Marekani
Mwanamke Mwislamu Mmarekani, Ilhan Omar ameweka historia kwa kuchaguliwa
kugombea kiti katika Bunge la Wilaya ya 60B jimbo la Minnesota nchini
MarekaniENDELEA
MAREKANI:IMAMU NA MSAIDIZI WAKE WAUAWA
Duru za habari zinaarifu kuwa, Imam Alala Uddin Akongi wa Msikiti wa Jamia wa Al-Furqan na msaidizi wake aliyetambulika kama Thara Uddin waliuawa kwa kufyatuliwa risasi jana Jumamosi walipokuwa wakitoka kuswali swala ya Adhuhuri katika barabara ya Ozone, mji wa Borough of Queens jimboni New York.
IMAMU MAULAMA AKONJEE
Imamu Maulama Akonjee, 55, aliwasili Newyork miaka miwili iliyopita kutoka Bangladesh.
Baraza la Mahusiano ya Kiislamu na Marekani limelaani mauaji hayo na kusema kuwa wawili hao mbali na kuwa viongozi wa kidini, walikuwa viongozi wa kijamii katika mji huo. Haya yanajiri wiki moja baada ya wanajeshi waliostaafu katika jimbo la Texas nchini Marekani kutishia kuwakata vichwa kwa mapanga Waislamu watakaoenda kutekeleza ibada ya swala katika Msikiti wa Al-Sahaabah mjini Wataunga jimboni hapo. Alia Salem, Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Mahusiano ya Kiislamu la Marekani, CAIR, katika eneo la Dallas sambamba na kulaani kitendo hicho, alisema baraza hilo limekuwa likipokea malalamiko kutoka kwa wasimamizi wa msikiti huo ambao wamekuwa wakitishiwa maisha kwa njia ya simu na watu wasiojulikana..
Watu wa asili ya Bangladesh mjini New York wamuomboleza Imam Akonjee
Ikumbukwe kuwa, katika miezi ya hivi karibuni vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu vimeongezeka mno nchini Marekani na barani Ulaya. Hivi karibuni Mkuu wa Baraza la Waislamu nchini Ujerumani (ZMD) alisema kuwa, kuna wasiwasi wa kuongezeka vitendo vya chuki dhidi ya Waislamu katika nchi hiyo ya bara Ulaya. Pamoja na kuwepo propaganda chafu dhidi ya Uislamu lakini idadi ya watu wanaosilimu na kuingia katika dini hii tukufu imekuwa ikiongezeka kwa kasi mno katika ulimwengu wa Magharibi.
No comments:
Post a Comment