Wanachuo Waislamu wa Chuo Kikuu cha jimbo la Wisconsin nchini Marekani
wameanzisha kampeni ya kugawa chakula kwa watu wasio na makazi wa mji wa
Madison ili kuwapa fursa ya kuujua Uislamu na kuuliza maswali kuhusiana
na dini hiyo ya Mwenyezi Mungu
Shirika la habari la IQNA limemnukuu Bi Najiha Khan, mkuu wa taasisi ya wanachuo Waislamu akisema kuwa, kushirikiana na watu wa dini nyinginezo na kuwaonesha kuwa Waislamu nao ni sawa na watu wengine, ni mbinu nzuri ya kupambana na propaganda chafu zinazoenezwa dhidi ya Waislamu.
Amesema, kampeni hiyo inawapa fursa ya kujibu maswali mbalimbali yanayoulizwa kuhusu Uislamu na kuondoa hofu waliyo nayo baadhi ya watu kuhusiana na Waislamu.
Mwaka jana (2015) viongozi kadhaa wa kidni wasio Waislamu, walitembelea Kituo cha Kiislamu mjini Madison na kuwakabidhi viongozi wa kituo hicho tambara kubwa lenye saini 400 ili kuonesha kuwa, Waislamu nao ni raia wa Marekani.
Waliotia saini tambara hilo kubwa walisema kuwa, lengo la hatua yao hiyo ni kutangaza uungaji mkono wao kamili kwa Waislamu na kwamba wako tayari kutetea haki za Waislamu na kukabiliana vikali na kampeni za kueneza chuki dhidi ya Waislamu.
Shirika la habari la IQNA limemnukuu Bi Najiha Khan, mkuu wa taasisi ya wanachuo Waislamu akisema kuwa, kushirikiana na watu wa dini nyinginezo na kuwaonesha kuwa Waislamu nao ni sawa na watu wengine, ni mbinu nzuri ya kupambana na propaganda chafu zinazoenezwa dhidi ya Waislamu.
Amesema, kampeni hiyo inawapa fursa ya kujibu maswali mbalimbali yanayoulizwa kuhusu Uislamu na kuondoa hofu waliyo nayo baadhi ya watu kuhusiana na Waislamu.
![]() |
Kuna jamii kubwa ya Waislamu nchini Marekani |
Mwaka jana (2015) viongozi kadhaa wa kidni wasio Waislamu, walitembelea Kituo cha Kiislamu mjini Madison na kuwakabidhi viongozi wa kituo hicho tambara kubwa lenye saini 400 ili kuonesha kuwa, Waislamu nao ni raia wa Marekani.
Waliotia saini tambara hilo kubwa walisema kuwa, lengo la hatua yao hiyo ni kutangaza uungaji mkono wao kamili kwa Waislamu na kwamba wako tayari kutetea haki za Waislamu na kukabiliana vikali na kampeni za kueneza chuki dhidi ya Waislamu.
No comments:
Post a Comment